JAMIE VARDY ASHIKWA UCHAWI KWA KUFUKUZWA KWA RANIERI AAMBIWA NDIE ALIECHOMA AFUKUZWE
BLOG NO 1 TANZANIA !! MIEZI tisa tu iliyopita kulikuwa na raha kubwa pale Leicester, lakini sasa kimenuka. Ni mwendo wa kumtafuta mchawi tu baada ya kufukuzwa kwa kocha aliyeipa ubingwa, Claudio Ranieri siku tatu zilizopita. Inasemekana baadhi ya wachezaji wa Leicester City walikuwa na kauli kubwa iliyotoa shinikizo kwa mmiliki wa Leicester City, Vichai Srivaddhanaprabha pamoja na mwanaye ambaye ni Makamu Mwenyekiti, Aiyawatt Srivaddhanaprabha kumfukuza kazi Muitaliano huyo. Mmoja kati ya wachezaji wanaotajwa kuwa nyuma ya kufukuzwa kwa Ranieri ni mshambuliaji mahiri wa timu hiyo, Jamie Vardy ambaye msimu uliopita alifunga mabao 24 yaliyosaidia kwa kiasi kikubwa kuipa ubingwa Leicester. Mwingine ni kipa wa timu hiyo, ...