Posts

Asasi 30 Afrika zalaani uvamizi Clouds

Image
                                         BLOG NO 1 TANZANIA !! Dar es Salaam. Asasi za kiraia 33 barani Afrika zimelaani kitendo cha kuvamiwa kwa studio za televisheni ya Clouds na kulazimisha maudhui yasiyostahili yarushwe hewani. Tamko la asasi hizo limetolewa ikiwa ni siku chache baada ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, (THBUB), Jukwaa la Wahariri (TEF) na Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kulaani kitendo hicho kinachodaiwa kukandamiza uhuru wa vyombo vya habari. Asasi hizo zinazohusika na utawala bora, demokrasia, haki za binadamu na uhuru wa habari zilikutana hivi karibuni mjini Kampala nchini Uganda katika mkutano uliokuwa ukizungumzia uhuru wa kujieleza na kupata habari. Tanzania kwenye mkutano huo iliwakilishwa na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu (THRDC) , miongoni mwa mijadala iliyotawala ni kukemea vitisho na vitendo vya kunyanyasa waand...

SOMA UJUMBE MZITO ALIOANDIKA RC MAKOND SIKU YA LEO

Image
                                                     BLOG NO 1 TANZANIA !! They came for the jews, I did not speak because I was not a Jew.

ETI ALIEMTISHIA BASTOLA MH: NAPE BASTOLA SIO ASKARI POLISI -MWIGULU NCHEMBA

Image
                                            BLOG NO 1 TANZANIA !! Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amesema mtu aliyemtishia kwa bastola aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye si askari wa Jeshi la Polisi, lakini ameshapatikana na atashughulikiwa kwa mujibu wa utaratibu wa ulinzi na usalama. Mwigulu alisema hayo baada ya kufungua mkutano wa kazi wa mwaka wa maofisa waandamizi wa polisi, makamanda wa mikoa na wakuu wa vikosi wa Jeshi la Polisi ambao unafanyika mjini hapa. “Ameshapatikana (aliyemtishia Nape) na atashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu za ulinzi na usalama ambazo zimekuwa zikifanyika ndani, lakini hazitangazwi,”alisema. Hata hivyo, Mwigulu alikataa kuelezea kwa undani kuhusu mtu huyo kwa kubainisha anatoka taasisi gani wala jina la mtuhumiwa kwa madai kuwa ni kwa sababu ya usalama wake. Baadhi ya taasisi za ul...

Siku Chache Baada ya Makonda Kuvamia Clouds,Mtangazaji wa Shilawadu Amepost Picha Hii ya Nape na Kuandika Maneno Tata..!!!

Image
                                                 BLOG NO 1 TANZANIA !! MTANGAZAJI na mwanachama wa Shirika la Wambeya Duniani ‘Shilawadu’, Soudy Brown leo ameweka picha ya kwanza mtandaoni baada ya kutoka likizo iliyosababishwa na sekeseke la kuvamiwa kwa kituo chao cha kurushia matangazo, Clouds Televisheni na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda.

LISSU AZIDI KUMCHARUKIA RAIS MAGUFULI HEBU FUATILIA HABARI HAPA!!

Image
                                            BLOG NO 1 TANZANIA !! Lissu azidi kumcharukia Magufuli, akerwa mtuhumiwa wa Range Rover zilizofichwa kwenye makontena ya mitumba kusota mahabusu siku 23 RAIS wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Tundu Lissu, ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, amesikitishwa na hatua ya Jeshi la Polisi –  kitengo cha Bandari kuendelea kumshikilia Ramadhani Mussa Hamisi Ukwaju, bila kumfikisha mahakamani ama kumwachia kwa dhamana. Ramadhani ndiye anayehusishwa na tukio la kusafirisha magari matatu ya kifahari aina ya Range Rover katika makontena ambayo taarifa zake zilionyesha mzigo huo ni nguo za mitumba, tukio lililofichuliwa na Rais Dk. John Magufuli alipofanya ziara ya kushtukiza katika Bandari ya Dar e s Salaam takriban wiki moja iliyopita. Lissu ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na pia Mnadh...

WANAJESHI 40 WAUAWA KWA MAPANGA DRC

Image
                                                BLOG NO 1 TANZANIA !! Wanamgambo nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wamewashambulia na kuwaua kwa kuwakatakata wanajeshi takriban 40 baada ya kuwavizia katika mkoa wa Kasai, katikati mwa nchi hiyo, maafisa wa serikali wamesema.Wapiganaji hao kutoka kundi la Kamwina Nsapu walishambulia polisi waliokuwa kwenye msafara.Maafisa sita wa pilisi waliowasiliana na Tshiluba waliachiliwa huru, rais wa bunge la jimbo la Kasai Francois Kalamba amesema.Machafuko jimbo la Kasai yalianza Agosti mwaka jana, pale maafisa wa polisi walipomuua kiongozi wa Kamwina Nsapu. Shambulio la Ijumaa lililenga msafara wa polisi waliokuiwa wakisafiri kati ya Tshikapa na Kananga. Gavana wa jimbo hilo Alexis Nkande Myopompa amesema uchunguzi umeanzishwa kuhusu mauaji hayo.Umoja wa Mataifa unasema watu 400 wameuawa na wengine 200,000 kuachwa bi...

FIFA kumlipa mshahara beki aliyevunjwa mguu

Image
                                                         BLOG NO 1 TANZANIA !! Geneva,Uswisi.