CHELSEA YANG'ANG'ANIWA TURF MOOR, SARE 1-1 NA BURNLEY



Mshambuliaji wa Chelsea, Diego Costa (kushoto) akimtoka kwa mbinde kiungo wa Burnley, Joey Barton katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Turf Moor mjini Burnley. Timu hizo zimetoka sare ya 1-1, Chelsea wakitangulia kwa bao la Pedro Eliezer Rodriguez Ledesma dakika ya saba, kabla ya Robbie Brady kuisawazishia Burnley dakika ya 24. Pamoja na sare hiyo, The Blues inaendelea kuongoza Ligi Kuu kwa pointi zake 60, ikifuatiwa na Tottenham na Arsenal zenye pointi 50 kila moja

Comments

Popular posts from this blog

MWANJALE AONGEZEWA SIKU NYINGIZE ZA MATIBABU