TORRES AUNUSURIKA KUFA UWANJANI, AKIMBIZWA HOSPITALI BAADA YA KUANGUKIA KICHWA VIBAYA
BLOG NO 1 TANZANIA !!

MSHAMBULIAJI Fernando Torres jana alikimbizwa hospitali
nchini Hispania baada ya kuumia kichwani. Torres aliuamia
baada ya kuingia dakika ya 65 akitokea benchi kuchukua
nafasi ya Kevin Gameiro.Mshambuliaji huyo wa zamani wa
Liverpool na Chelsea, kwanza aliumia mapema tu katika
mchezo wa Liga usiku wa jana dhidi ya Deportivo La Coruna
Uwanja wa Manispaa ya Riazor mjini La Coruna, timu hizo
zikitoka sare ya 1-1.Aliangukia kichwa uwanjani baada ya
kugongana na Alex Bergantinos na kuwashitua wachezaji
wenzake baada ya hali yake kubadilika. Gabi alipigwa na
Torres wakati akijaribu kumzuiaa asiueze ulimi.Wachezaji wa
Atletico Madrid wakijaribu kumzuia Fernando Torres
asiumeze ulimi baada ya kuumia jana, Hata hivyo, Atletico
Madrid imethibitisha mchezaji wake huyo anaendelea vizuri
hospital. Katika mchezo huo, Florin Andone alianza
kuwafungia wenyeji dakika ya 13, kabla ya Antoine
Griezmann kuisawazishia Atletico dakika ya 68.Baadaye
Torres mwenyewe akaandika kwenye akaunti yake Twitter
kuwaambia mashabiki wasiwe na wasiwasi juu ya hali yake:
"Asante nyingi kwa wote kwa kunifuatilia hali yangu na kwa
meseji zenu za kunifariji. Ilikuwa ni hofu tu. Natumai kurejea
karibuni!,"
Comments
Post a Comment