Posts

Showing posts from February, 2017

TRUMP AANZA KUMCHOKONOA OBAMA ASEMA NDIE ANAEPANGA MAANDAMANO DHIDI YAKE MAREKANI SOMA HABARI HIO HAPA!!

Image
                                            BLOG NO 1 TANZANIA !!

Waziri Nape: Sikupinga vita dhidi ya biashara ya dawa za kulevya bali nilishauri busara itumike

Image
                                                     BLOG NO 1 TANZANIA !! Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye ametoa ufafanuzi juu ya kauli iliyonukuliwa ikionyesha kuwa alipinga vita dhidi ya dawa za kulevya iliyoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. Amedai kuwa hakupinga vita hiyo bali alitaka busara itumike kwa washukiwa. Waziri Nape alitoa ufafanuzi huo katika kipindi cha dakika 45 cha ITV, alipoulizwa swali na mtangazaji wa kipindi hicho kutaka kujua kuhusu kauli yake iliyoonesha kupinga utaratibu uliotumika wa kuwakamata au kuwapata watuhumiwa wa dawa za kulevya. “Niseme kwanza ilitokea nilikuwa na mkutano na waandishi wa habari, ukienda leo ukanitaja Nape ukaniambia baada ya siku mbili njoo kituoni, hata kama nilikuwa na madawa ya kulevya nyumbani kwangu hivi unayakutaje?  ‘Kwasababu ...

Ally Kiba, Diamond wakabidhiwa Serengeti Boys wahakikishe inashinda mechi zao zote!!

Image
                                           BLOG NO 1 TANZANIA !! Akitangaza kamati hiyo inayoundwa na wanahabari, viongozi wa kampuni na wasanii Waziri wa Habari, Utamaduni Sana’a na Michezo Nape Nnauye amesema jukumu kubwa la kamati hiyo ni kuhakikisha wananchi wanashirikishwa kwenye maandalizi ya timu hiyo. “Tumeshamiria kuona timu hii inafanya maandalizi makubwa na nimeongea na Malinzi asubuhi hii yuko Morocco akiweka sawa masuala ya kambi ya vijana,”amesema. Kamati hiyo itakuwa chini ya uenyekiti wa mwanahabari mkongwe Charles Hillary na katibu ni katibu mkuu wa TFF, Mwesigwa Selestine. Wajumbe wa kamati hiyo ni wanamuziki Ally Kiba na Diamond Platnumz wengine ni Beatrice Singano, Ruge Mutahaba, Maulid Kitenge, Erick Shigongo, Hassan Abbas na mwanamitindo Hoyce Temu. Serengeti Boys imefuzu kucheza fainali za vijana Afrika nchini Gabon Mei 24- Juni 5...

MAKONDA ALALAMIKA KUTUPIWA JINI NA WATU 12 ALIOWATAMBUA!! SOMA HABARI HIO HAPA!!

Image
                                           BLOG NO 1 TANZANIA !! Katika mapambano yanayoendelea ya watu wanaojihusisha na biashara ya dawa za kulevya pamoja na watumiaji, kuna watu 12 waliokuwa wamepanga njama za kunitupia majini lakini hawakufanikiwa kutokana na kinga ya maombi kutoka kwa viongozi wa dini. Hayo yalisemwa juzi na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam , Paul Makonda alipokuwa katika semina ya  Masheikh , wanazuoni, maimamu na walimu wa Quran Tanzania kupitia jumuiya ya walimu wanaosomesha Quran Tanzania (JAWAQUTA). Makonda alisema waumini hao 12 waliandaa mbuzi mweupe ili kumtoa kafara na yeye alifanikiwa kuwatambua kupitia mtandao  wake . Aidha alisema, haamini kama waumini hao ni wa dini ya kiislamu, bali ni kundi la  watu waliokuwa  wamevalia kanzu kwa utambulisho huo na kwamba huenda walitumika kuwalia watu fedha zao. Pia aliwaomba viongoz...

Kim Jong Un alitoa amri ya kuuawa kwa kaka yake

Image
                                                      BLOG NO 1 TANZANIA !! WIZARA mbili za Korea Kaskazini zilipanga mauaji ya Kim Jong Nam kutokana na amri ya kaka yake wa kambo, kiongozi wa nchi hiyo Kim Jong Un, shirika la kijasusi la Korea Kusini limesema. Wabunge huko Seoul, ambao walipewa taarifa ya maafisa wa kijasusi wa nchi hiyo, walisema Wizara za Mambo ya Nje na ile ya Usalama wa taifa za Korea Kaskazini ziliwapa kazi washukiwa wawili wa kike katika mauaji ya Kim. “Mauaji ya Kim Jong Nam ni tendo la kigaidi lililoamriwa na Kim Jong Un,” mbunge wa Korea Kusini Kim Nyung-kee alisema kupitia televisheni. Operesheni ilifanywa na makundi mawili ya mauaji na moja likiwa linatoa msaada.” Korea Kaskazini imekuwa ikikana kuhusika na mauaji ya Kim Jong Nam na imekuwa ikivishutumu vyombo vya habari vya Korea Kusini kwa kuandika “habari za...

MBUNGE AOMBA APIGWE MAWE NA WANANCHI -TANGA

Image
                                              BLOG NO 1 TANZANIA !! Mbunge wa Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani maarufu Profesa Majimarefu, ametoa ruhusa kwa wakazi wa jimbo lake kumwadhibu kwa kumpiga mawe iwapo atashindwa kutekeleza ahadi alizoahidi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa 2015. Majimarefu aliyasema hayo wakati akizungumza kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara na wananchi wa Vijiji vya Kwemshai, Ngulu na Mlungui, katika ziara yake jimboni mwake. Alisema licha ya kuwa nje ya nchi kwa matibabu, lakini baada ya afya yake kuimarika amerejea nchini akiwa tayari kutatua kero za umma. Aidha, amewaomba wapigakura wake kuendelea kushirikiana naye huku wakimpatia muda kumwezesha kuwatatulia kero hizo. “Nawashukuru kwa kuniombea pale nilipokuwa nikiugua, nilikuwa nje ya nchi kwa matibabu sala zenu zimeniwezesha kuungana nanyi leo,” alisema...

AKUTWA ANAFANYA MAPENZI NA MAITI YA MWANAE WAKATI WATU WAMELALA MATANGA,WANANCHI WAMPIGA MPAKA KUMSABABISHIA KIFO

Image
                                             BLOG NO 1 TANZANIA !! Mwanaume mwenye umri wa miaka 45 kutoka Kenya amepigwa na Wananchi baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na maiti ya Mtoto wake aliyekuwa na umri wa miaka 15 ambapo ripoti ya K24 TV imeripoti tukio hilo kutokea kwenye kijiji cha Kiwanja Ndege  kaunti ndogo ya Kuresoi Kaskazini. Mashaidi wanasema baada ya mtoto kufariki kutokana na uvimbe wa Ubongo kichwani walihifadhi mwili kwenye chumba cha pekee lakini mida ya SAA nane usiku baba wa mtoto huyo aliamka na kwenda katika chumba hicho na ndipo alipokutwa akiwa anafanya mapenzi na maiti hiyo kitendo ambacho kiliwakasirisha wananchi na kuanza kumpiga hadi kupelekea kifo chako

Zitto Kabwe Ashindwa Kuzuia Hisia Zake Sakata Kushikiliwa Godbless Lema…Ataka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu Iwajibishwe

Image
                                           BLOG NO 1 TANZANIA !!     Kitendo cha Mbunge wa Arusha mjini kukaa rumande kwa zaidi ya miezi minne sasa pasipo kupatiwa dhamana kimemfanya Mbunge wa Kigoma Mjini Mh. Zitto Zuberi Kabwe kushindwa kuzuia hisia zake na kutaka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali iwajibishwe Katika mtandao wake wa kijamii Mh. Zitto amedai kuwa kitendo cha  Mbunge huyo ambaye ni muwakilishi wa wananchi kunyimwa dhamana  ni siasa za ukomoaji ambazo zinajenga chuki kwenye jamii na chuki huwa zinazaa visasi. “Haitoshi majaji kukemea Ofisi ya DPP, Mfumo wetu lazima uweke uwezo wa waendesha mashtaka wa aina ya kesi ya Mbunge wa Arusha Mjini kuwajibishwa. Wanasheria tazameni namna ya kuwajibisha ofisi ya DPP kwa uonevu wa makusudi dhidi ya wananchi” Ameandika Zitto Kabwe Hata hivyo kauli hiyo ya Zitto imekuja mapema leo baada ya ...

NYUMBA YA MAMA WEMA YAVAMIWA USIKU WAFANYIWA FUJO,MEYA AFIKA NA KUSEMA WAMEGUNDUA KITU WAWEKEWA ULINZI MKALI

Image
                                              BLOG NO 1 TANZANIA !! Nyumba ya mama Wema Sepetu, Mariam Sepetu, iliyopo Sinza Mori jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia jana imepigwa mawe juu ya bati kwa muda wa saa moja na nusu. Kutokana na tukio hilo viongozi wa Chadema wamechukua hatua ya kuweka ulinzi mkali nyumbani hapo na kuzungumza kuwa wamegundua kitu ambacho hawatakiweka wazi kwa sasa. Baada ya tukio hilo kutokea mama Sepetu aliwasiliana na mwanae Wema Sepetu pamoja na viongozi wa Chadema, ambapo Meya wa Ubungo, Boniface Jacob alifika na kuangalia hali ya mama huyo na kuamua kuweka ulinzi. ”Tumeshaangalia mazingira yote tumegundua kitu ambacho hatuta kiweka wazi kwa sasa ila tutaweka ulinzi mkali na atakaye jaribu shauri yake hatuta kubali suala hili liendelee kumkuta kamanda wetu na mimi mara kwa mara nitafika kuangalia mazingira”  amezung...

Freddie Ljungberg aitosa Arsenal na kutua Ujerumani

Image
                                               BLOG NO 1 TANZANIA !! London, England. STAA wa zamani wa Sweden,Freddie Ljungberg amekikacha kibarua chake cha kukinoa kikosi cha vijana cha Arsenal cha U-15 na kutua Wolfsburg kwenda kuwa mmoja kati ya wasaidizi wa Andries Jonker ambaye ametangazwa kuwa kocha mkuu mpya wa klabu hiyo ya Ujerumani inayosuasua kwenye ligi ya Bundesliga. Ljungberg,39,alirejea Arsenal msimu uliopita baada ya kustaafu mwaka 2014 na kupewa jukumu la kuwa kocha wa kikosi cha vijana cha U15 kibarua ambacho alikifanya vizuri na kumvutia Jonker aliyekuwa akihudumu kama mkuu wa akademi ya Arsenal. Ljungberg alijiunga na Arsenal mwaka 1998 akitokea Halmstads BK.Aliichezea Arsenal kwa miaka minane akifunga mabao 71 katika michezo 313.Pia aliisaidia klabu hiyo ya kaskazini mwa London kushinda vikombe viwili ya FA na vikombe viwili ...

Mkuu wa majeshi afutwa kazi Gambia

Image
                                              BLOG NO 1 TANZANIA !! Rais wa Gambia Adama Barrow amemfuta kazi mkuu wa majeshi Jenerali Ousman Badjie. Jenerali Badjie alitangaza utiifu wake kwa rais aliyeondoka madarakani Yahya Jammeh baada ya uchaguzi wa Disemba ulioleta vuta nikuvute. Hata hivyo, chini ya amri yake, jeshi halikutoa msaada wowote pindi vikosi kutoka nchi za Afrika Magharibi vilipoingia nchini Gambia mwezi jana. Vikosi hivyo vilifanikiwa katika kumshawishi bwana Jammeh kukubali kushindwa na kuondoka nchini.

LEICESTER CITY YAIPASUA LIVERPOOL 3G YAIKANDAMIZA TAIRI ZA BAJAJI 3-1

Image
                                               BLOG NO 1 TANZANIA !!

MKUU WA SHULE YA SEKONDARI AJINYONGA...CHANZO UPWEKE BAADA YA ULEVI

Image
                                                BLOG NO 1 TANZANIA !! MKUU wa Shule ya Sekondari Tumuli katika Wilaya ya Mkalama, mkoani Singida, Richard Makala (58) amejinyonga kwa kamba kutokana na kile kinachodhaniwa kuelemewa na upweke. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, Debora Magiligimba, amesema mjini Singida kuwa, Makala alijinyonga jana saa 1 asubuhi. Ameeleza kuwa Makala alikutwa amejinyonga kwa kutumia kamba iliyotengenezwa kwa vipande vya chandarua iliyofungwa juu ya mti umbali wa mita 130 kutoka nyumbani kwake. Amesema, chanzo cha tukio hilo hakijajulikana na kwamba hakuna mtu au watu wanaoshikiliwa kutokana na tukio hilo na kuongeza kuwa polisi inaendelea na upelelezi kubaini kilichomsibu mwalimu huyo. Hata hivyo, Mjumbe wa Bodi ya shule hiyo, Mabruki Ng’ui amelisema mwalimu huyo alikuwa anaishi peke yake kwa muda mrefu baada y...

WATANZANIA WAMJARIBU RAIS MAGUFULI KUPITIA MAKONDA

Image
                                                  BLOG NO 1 TANZANIA !! Rais John Magufuli alipata kueleza kuwa yeye hajaribiwi, hata mimi naamini kuwa Rais wangu hajaribiwi. Rais wangu Magufuli yupo tofauti sana, mwenyewe alishasema hivyo. Ninachompendea Magufuli wetu ni kuwa hajui kuremba. Hana kawaida ya kulazimisha nyekundu ionekane kijani. Hapana Rais Magufuli yupo tofauti sana. Kwake nyekundu ni nyekundu na kijani ni kijani. Lipo jambo linalotawala sasa hivi, ni kuhusu uhalali wa cheti cha kidato cha nne ambacho Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alikitumia kusomea elimu ya juu. Hapa ndipo watu wanataka kumjaribu Rais wangu Magufuli. Kwamba afunike kombe mwanaharamu apite ili watu waseme Makonda ni invulnerable prince, yaani mwanamfalme asiyeguswa. Rais Magufuli siyo kwamba hajui haya, anajua sana, amekaa kimya kama mtu mzima. Bila shaka yupo kwe...

MAHARUSI WA AJALI YA KUSOMBWA NA MAJI YA MAFURIKO KUZIKWA KESHO ARUSHA

Image
                                                  BLOG NO 1 TANZANIA !! Arusha. Maharusi Munisi Roy (25) na Nembrice Munyaga (20) waliofariki kutokana na mafuriko Februari 24, wanatarajiwa kuzikwa kesho katika kijiji cha Ilkisongo Kata ya Sambasha wilayani Arumeru mkoani Arusha.  Maharusi hao, walifariki juzi baada ya kuzolewa na mafuriko wakiwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Premio, pamoja na ndugu wengine watatu. Diwani wa kata ya Sambasha, Roy Sabaya amesema marehemu hao watazikwa baada ya kukamilika taratibu za mazishi.

Serikali Yasema Makonda Aliingizwa ‘Mkenge

Image
             BLOG NO 1 TANZANIA !! Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itamchukulia hatua muwekezaji aliyetoa ardhi kwa serikali ya mkoa wa dar es Salaam kwa ajili ya ujenzi wa viwanda, kwa madai kuwa ardhi aliyoitoa siyo yake. Waziri wa wizara hiyo, William Lukuvi, ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa muwekezaji huyo aliidanganya serikali pamoja na kumdanganya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, ambaye ndiye aliyekabidhiwa eneo hilo kwa niaba ya serikali. Mbali na kosa la kuidanganya serikali, Lukuvi pia amesema atamchukulia hatua mfanyabiashara huyo kwa kumiliki ardhi kinyume cha sheria. Kuhusu Mkuu wa Mkoa , Paul Makonda, Lukuvi amesema tayari amekwishafanya naye mawasiliano na kumuelewesha kuwa alidanganywa kwa kuambiwa kuwa anapewa eneo kwa ajili ya viwanda, huku eneo lenyewe likiwa ni mali ya serikali. Siku ya Jumanne wiki iliyopita Makonda alikabidhiwa ekari 1500 za ardhi na Mk...

HII Ndiyo DNA ya Kitamaduni Kabisa Yenye Ukweli 90% Kujua Kama Mtoto ni Wako Au Umebambikiziw

Image
                                                BLOG NO 1 TANZANIA !! Hapo nyuma nilikuwa nikiambiwa kuwa Wazee ni dawa na hazina hasa katika kutupatia Maarifa sisi Vijana na Wajukuu zao nilikuwa sitaki kuamini na kuna wakati hata nilikuwa nikimwona tu Mtu Mzee au Bibi basi nawapuuza tu nikiamini kwamba hawana jipya tena. Hali hii ilibadilika taratibu baada ya kuanza sasa kupenda kukaa na Wazee mara kwa mara ili niweze kuchota hekima na busara zao na kwa kweli tokea nianze kurudisha imani yangu kwa Wazee naona nimefaidika mno katika kupata Elimu dunia ambayo wengi wetu hatuna na tumebaki tu kujikita katika Elimu zetu hizi za Kitaaluma tukidhani kuwa pekee ndizo zitatukomboa Kifikra. Pamewahi kuwa na nadharia kwamba akina Babu na Bibi wao huweza kujua Mtoto mchanga aliyezaliwa leo kama ni Mjukuu wao kweli au labda Mtoto wao amebambikiwa huyo Mtoto na Mama yake kutokan...

VICENT BOSSUE AKAMATWA UCHAWI YANGA MJENGA MAKUNDI, NA NDIE ALIYE....................

Image
                                                 BLOG NO 1 TANZANIA !!                                           B eki wa kimataifa wa Togo Vicent Bossue alikuwa anaiwakilisha timu yake ya taifa kwenye michuano ya AFCON  huko Gabon alivyorudi alikuta timu Iko kwenye Maandalizi ya mechi dhidi ya Ngaya club ya Cammoro alifanya mazoezi na timu lakini hakujumuishwa timu iliyosafiri kwenda Commoro.  Yanga wakaenda kumaliza shughuli huko Commoro Kwa kuwafunga magoli matano Kwa moja tena kwao wakarahisisha mechi ya marudiano ambapo Bossue akajumuishwa kwenye program ili awe fiti kuelekea mechi ya watani iliyochezwa juzi.   Baaada ya mechi ya marudiano dhidi ya Ngaya club., Mabingwa hao watetezi wa ligi kuu ya Vodacom  wakaenda kuweka...

BREAKING NEWS!! MAHAKAMA YATUPILIA MBALI RUFAA YA SERIKALI LEMA KUPEWA DHAMANA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA!!

Image
                                              BLOG NO 1 TANZANIA !! Mahakama ya Rufaa imetupilia mbali mapingamizi (rufaa) ya Serikali dhidi ya maamuzi ya Mahakama Kuu kwa msingi kwamba hayana mashiko na kuiagiza Mahakama Kuu kuendelea na utaratibu wake wa kutoa haki ya dhamana mapema iwezekanavyo! Kutoka kushoto (viongozi wa CHADEMA): Mwenyekiti Mkoa wa Arusha, Amani Golugwa; Katibu Mkuu Vincent Mashinji, Mwenyekiti Taifa Freeman Mbowe na Katibu wa Mkoa wa Arusha Kalisti Lazaro.

Jenerali Ulimwengu Aiomba Mahakama Imuunganishe Katika Kesi Ya Mbowe Dhidi Ya Makonda

Image
                                             BLOG NO 1 TANZANIA !! Mwanahabari nguli Jenerali Ulimwengu, leo anatarajia  kuwasilisha maombi Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akiomba kuungana na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe  katika kesi ya katiba iliyofunguliwa hivi karibuni. Ulimwengu anaomba kuunganishwa katika kesi ya katiba namba 1 ya 2017 kama mdai dhidi ya wadaiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam na Ofisa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. “Maombi ya kumuunganisha yameandaliwa na kesho(leo) yatakuwa mahakamani kuomba naye awe mdai. Anaomba kujiunga kwa kuwa mambo anayopigania Mbowe naye ana maslahi nayo kwa sababu ni mambo muhimu ya katiba,” alisema mmoja wa jopo la Mawakili kutoka Kurugenzi ya Katiba Sheria na Haki za Binadamu ya Chadema...